Home » 2017 » December » 25

SINBAD BAHARIA NA SAFARI ZAKE SABA



SEHEMU YA KWANZA

Hindubad mbeba mizigo

KATIKA utawala wa Khalifa Haroun Rashid, aliishi katika jiji la Bagdad maskini aitwaye Hindbad. Siku moja, wakati hali ya hewa ilikuwa ya joto kali, Hindbad alipata tenda ya kubeba mzigo mzito kuupeleka mbali sana kutoka sehemu hiyo ya mji ambako aliishi. 

Alitaabika na joto na uchovu sana, na akiwa bado na safari ndefu ya kwenda, aliingia katika mtaa mmoja ambapo hewa yenye ubaridi mzuri ilipiga juu ya uso wake, na sehemu za kando ya barabara za mtaa huo zilikuwa zikinyunyiziwa na marashi ya waridi.

Alifurahi kupata mahali pa kupumzika kama pale, akaweka mzigo wake, na akaketi kando yake, karibu na nyumba kubwa.
M ... Read more »

Category: Stories & Entertainment | Views: 881 | Added by: badshah | Date: 25/Dec/2017 | Comments (8)